Monday 20 February 2012

LEO MABIBI NA MABWN TUKO KWA SECTOR YA MAPISHI




Buns

MAPISHI YA BUNS

Mahitaji
  1. unga vikombe 3
  2. Hamira vijiko viwili vya chai
  3. mafuta vijiko viwili vya chakula
  4. mtindi vijiko vitatu vya chakula
  5. yai moja
  6. chumvi nusu kijiko cha chai
  7. maziwa fresh kikombe kimoja
jinsi ya kuandaa
  • changanya hamira ,sukari na maji kidogo 
  • weka unga ,chumvi,mafuta,yai na maziwa mtindi kwenye mchanganyiko wako
  • changanya vizuri mchanganyiko ongeza maziwa fresh ya uvuguvugu
  • acha unga uumuke kwa mda wa saa 1
  • chukua unga wako kata kata madonge ya saizi na weka kwenye tray
  • chukua brush paka mafuta juu ya madonge yako
  • weka kwenye oven kwa mda wa dk 20
  • baada ya dk hizo toa mikate yako na iko tayari kwa kuliwa
  • inaweza kuliwa na chai au hata juice 
 haya mdau wangu enjoy mapishi ya leo ,jifunze kujaribu kwani kutakusaidia cku ya kwanza unaweza ukakosea bt cku nyingine utashangaa utakavokuwa expert ,penda kujaribu vitu vizuri ..

nawapenda wote wadau wangu
its me blogger
Wa Kaumo
<3 <3 <3

1 comment:

  1. kwa kweli yaonekana mapishi mazuri ntajaribu na mie ,,

    ReplyDelete